Saturday, June 18, 2011

Chiluba Afariki Dunia Ghafla...



Aliyekuwa Rasi wa pili wa Zambia, Frederick Jacob Titus Chiluba (68), amefariki dunia ghafla usiku wa kuamkia leo nchini Zambia. Chiluba, ambaye aliiongoza Zambia kuanzia mwaka 1991 - 2002, hadi jana mchana inadaiwa alionekana mwenye afya njema, lakini ilipofika saa 6 usiku aliugua ghafla na kuaga duania. Hadi sasa hakuna taarifa zaidi zilizotolewa kuhusu sababu za kifo chake.

No comments:

Post a Comment